Mkurugenzi wa taasisi ya Darul Qur’ani ya mji wa Nasiriyya Raad Adnan ameliambia shirika la habari la IQNA kwamba kongamano hilo limenza leo asubuhi na kwamba linahudhuriwa na wapenzi wa Qur’ani kutoka mikoa ya Baghdad, Misan al Muthanna, Najaf na Karbala.
Amesema kongamano hilo linajadili sababu za umma wa Kiislamu kuwa mbali na Qur’ani na njia za kuondoa tatizo hilo. Amesema maudhui nyingine inayojadiliwa ni fasaha na balagha ya Qur’ani Tukufu.
Raad Adnan ameongeza kuwa miongoni mwa ajenda za kongamano hilo ni vikao vya kiraa ya Qur’ani Tukufu itakayowashirikisha makarii mashuhuri wa mikoa inayoshiriki katika kongamano hilo. 833708