IQNA

Msikiti wa Nurul Yaqin wa Indonesia katika Picha

Kituo cha Kiislamu cha Msikiti wa Nurul Yaqin huko Palu, Indonesia, kimejengwa kwa muundo wa kawaida sana lakini wenye utulivu unaoendana na mazingira yenye maji.

Wasanifu majengo wa Jakarta Dave Orlando na Fandy Gunawan ndio waliochora ramani ya msikiti huo ambapo wametumia zege, tofali na terrazzo ya samawati ili kuunda muundo wa kawaida lakini  maridadi kwa ajili ya ibada. Ukumbi wa Sala una vifuniko vya mapambo na mpasuo zinazoruhusu mwanga wa asili na hewa, wakati sakafu ya terrazzo inaashiria Sala isiyo na mwisho.