IQNA

Kazi bora 300 za kaligrafia ya Qur'ani kuonyeshwa Madina

17:37 - February 14, 2011
Habari ID: 2080922
Wasanii bora wa kaligrafia ya Qur'ani kutoka ulimwengu wa Kiislamu wamewasilisha kazi 300 za sanaa hiyo katika kamati inayoshughulikia kongamano la wasanii hao litakalofanyika katika mji mtakatifu wa Madina.
Shirika rasmi la habari la Bahrain limeripoti kuwa kuwa kamati za kielimu na ile ya majaji wa kongamano la wanakaligrafia bora wa Kiislamu zimekubali kazi 230 kati ya kazi zote 300 zilizowasilishwa.
Kongamano hilo limepangwa kufanyika yapata miezi miwili ijayo likisimamiwa na Kituo cha Qur'ani cha Mfalme Fahad mjini Madina na litawashirikisha wanakaligrafia wa Qur'ani kutoka ulimwengu wa Kiislamu.
Miongoni mwa malengo ya kongamano hilo ni kubainisha ujumbe muhimu wa wanakaligrafia wa Qur'ani Tukufu, kueleza uzoefu wao katika masuala ya Qur'ani, kuimarisha uhusiano baina ya wasanii hao na kuwaenzi. 747487
captcha