IQNA

Aya za Qur'ani zatarjumiwa kwa lugha ya ishara Saudia

12:18 - February 24, 2011
Habari ID: 2085714
Hatua za mwisho za kutarjumi na kutafsiri baadhi ya aya za Qur'ani kwa lugha ya ishara zimekamilika katika Kituo cha Qur'ani cha Mfalme Fahd katika mji mtakatifu wa Madina.
Kwa mujibu wa tovuti ya Mohet, kituo hicho kimesema kuwa Suratul Fatiha na sura 20 za mwisho za Qur'ani zimetarjumiwa na kufasiriwa kwa lugha ya ishara. Iwapo mradi huo utafanikiwa, utaendelezwa katika aya nyingine za Qur'ani Tukufu.
Muhammad bin Salem Shadid al Ufi mkurugenzi wa kituo hicho amesema kuna mpango wa kuzindua program za kompyuta kuhusu Qur'ani Tukufu maalumu kwa wanaotumia lugha ya ishara.
752440
captcha