Kwa mujibu wa gazeti la as-Sharq la Qatar mashindano hayo yameandaliwa na Idara ya Shughuli za Vijana ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Turathi ya nchi hiyo.
Mashindano hayo yanafanyika katika vitengo vinne vya hifdhi ya Qur'ani, sheria za usomaji na tajwidi ya Qur'ani, tafsiri na hadithi.
Akizungumzia suala hilo Jamal Faiz, mkuu wa kitengo cha shughuli za utamaduni cha Idara ya Shughuli za Vijana cha Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Turathi ya Qatar amesema vijana wote wanachama wa vilabu vya michezo na vituo vya vijana wanashiriki katika mashindano hayo. 755242