Kongamano hilo litajadili athari za sinema katika mwamko unaoshuhudiwa katika nchi za Kiarabu. Natija ya kongamano hilo itawasilishwa katika sherehe za kufunga Tamasha ya Kimataifa ya Fajr ya Filamu itakayofanyika Tehran.
Wataalamu 30 na wazungumzaji kutoka Kuwait, Misri, Algeria, Tunisia, Uturuki, Iraq, Yemen, Morocco na Uingereza pamoja na wanadiplomasia wa nchi kadhaa pia watashiriki.
Katibu wa kongamano la ‘Mwamko wa Kiislamu na Sinema’ ni Mohammad Khazaee.
Awamu ya 30 ya Tamasha ya Kimataifa ya Fajr ya Filamu itaanza Februari Mosi mjini Tehran. 940645