Akizungumza katika hafla ya kufunga Mashindano ya 44 ya Qur’ani ya Kikosi cha Nchi Kavu cha IRGC mapema wiki hii, Brigedia Jenerali Mohammad Karami alisema: “Hatupaswi kurudi nyuma mbele ya vitisho vya maadui, na bila shaka, silaha yenye nguvu tuliyo nayo katika njia hii ni Qur’ani.”
Aliongeza: “Upande wa batili umeingia uwanjani kwa nguvu zote, lakini hatupaswi kuogopa vitisho hivi wala kurudi nyuma, kwa sababu tunategemea Qur’ani, na huu ni ahadi ya Mwenyezi Mungu kwamba ushindi uko upande wa haki.”
Kamanda huyo wa ngazi ya juu alisisitiza kuwa Qur’ani ni nuru, kitabu cha maisha, na “mwanga wetu wa kuongoza katika nyanja zote.”
Alisema Qur’ani ni mwongozo bora wa maisha, na “tunapaswa kutafuta msaada kutoka katika kitabu hiki cha kimungu katika kila kipengele cha maisha ya binadamu, ikiwemo uchumi, utamaduni, jamii na mahusiano ya kijamii.”
“Ukiifahamu Qur’ani, basi dunia nzima ni yako, na hofu haitapata nafasi mioyoni mwetu. Ikiwa vikosi vya nchi kavy vya IRGC vitakuwa vya Qur’ani, vitakuwa na uwezo wa kusimama katika hali ngumu zaidi, kwa sababu ahadi ya kweli ya Mwenyezi Mungu katika Qur’ani ni kwamba mkimsaidia katika dini, Yeye mwenyewe atakuwa msaidizi wenu katika hali ngumu.”
Akitoa shukrani kwa waandaaji wa mashindano na ushiriki wa washiriki, alisema: “Mtindo, tabia na nia ya wasomaji ni muhimu; tunapaswa kutumia fursa hii kueneza utamaduni wa Qur’ani ili Kikosi cha Ardhi cha IRGC kiwe kikosi cha Qur’ani.”
Akikumbusha kuwa Qur’ani ni muujiza na Neno la Mungu, Jenerali Karami aliongeza: “Lazima tuchukue hatua katika ulingo wa kueneza, kutangaza na kuinua Qur’ani. Kutumia fedha kwa ajili ya Qur’ani ni aina ya uwekezaji, na msaada wenye nguvu zaidi ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu; tukimtegemea Yeye, tutashinda.”
3494862