IQNA

Haram ya Imam Ridha AS katika mkesha wa kukumbuka Kuzaliwa kwa Imamu wa Tisa wa Shia

IQNA – Haram ya Imam Ridha (AS) huko Mashhad ilipambwa kwa maua kabla ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Imam Jawad (AS), Imam wa tisa wa Shia na mtoto wa Imam Ridha (AS). Maelfu ya watu waliadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mtukufu huyo tarehe 22 Januari 2024.

Tarehe 10 Rajab miaka 1250 iliyopita,  alizaliwa Imam Muhammad Taqi mmoja wa watu wa Nyumba Tukufu ya Bwana Mtume SAW katika mji mtakatifu wa Madina.

Imam Taqi Al-Jawad (as) alichukua jukumu la kuongoza Umma wa Kiislamu baada ya kuuawa shahidi baba yake yaani Imam Ridha (AS). Mtukufu huyo alikuwa maarufu kwa lakabu ya 'Jawad' yenye maana ya mtu mkarimu mno, kutokana na ukarimu wake mkubwa. 

 

Source: news.razavi.ir