Ufunguzi wa Mashindano ya 7 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Port Said-PICHA
IQNA - Toleo la 7 la Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Port Said yalifunguliwa tarehe 2 Februari 2024, katika mji huo wa Misri huku maafisa wa nchi na washindani wakihudhuria.
Mashindano hayo yameandaliwa katika kategoria za kuhifadhi Qur'ani Tukufu na kusoma Ibtihal. Toleo la mwaka huu limepewa jina la qari maarufu wa Misri Sheikh Shahat Muhammad Anwar (1950-2008).