IQNA

Kisomo cha Mbinguni: Msikilize Sheikh Al-Zanati akisoma aya za awali za Surah Al-Qaria

IQNA- Kinachofuata ni usomaji wa aya 1-3 ya Surah Al-Qaria na qari wa Misri Saeed Abdul-Samad Al-Zanati.

Mtume Muhammad (SAW) alisema wakati mmoja kwamba kuisikiliza Qur'ani Tukufu humletea mja thawabu za Mwenyezi Mungu, huku kila herufi ikisikika ikistahiki tendo jema kwa msikilizaji, na kumpandisha msikilizaji katika safu ya wale wanaosoma maandiko matukufu na kupaa kuelekea mbinguni. 
Shirika la habari la IQNA limeratibu na kutoa mfululizo unaoitwa "Kisomo cha Mbinguni," wenye kumbukumbu za kuvutia za wasomaji maarufu Qur’ani Tukufu.