IQNA

Shakhsia ya Imam Hussein (as) kubainishwa katika kikao cha India

17:05 - June 19, 2012
Habari ID: 2350037
Pande mbalimbali za fadhila za Imam Hussein (as) zitachunguzwa na kubainishwa katika kikao ambacho kimepangwa kufanyika siku ya Jumapili Juni 24 katika mji wa Ghazi Pur katika Jimbo la Uttar Pradesh nchini India.
Kikao hicho kitafanyika kwa mnasaba wa maadhimisho ya kuzaliwa Imam huyo mtukufu (saw). Lengo la kikao hicho ambacho kimeandaliwa na Jumuiya ya Ja'fari ya eneo la Zangipur limetajwa kuwa ni kuwabainishia wakazi wa jimbo hilo shakhsia ya Imam Hussein (as).
Watu watakaozungumza katika kikao hicho ni pamoja na Hujjatul Islam Dhulfiqar Ali mmoja wa wanafunzi wa Jamiatul Mustafa (saw) al-Alamiya.
Washairi mashuhuri wa India wamealikwa kushiriki katika kikao hicho kwa kusoma mashairi ya kumsifu Imam Hussein (as). 1032874
captcha