IQNA

Fadhila za Bibi Fatuma (as) zabainishwa nchini Tanzania

17:19 - June 20, 2012
Habari ID: 2350820
Fadhila za kiakhlaqi na maisha ya Bibi Fatma (as) zimebainishwa katika semina ya siku tatu iliyofanyika hivi karibuni katika mji wa Singida nchini Tanzania. Semina hiyo imeandaliwa na Taasisi ya Bilal Muslim.
Semina hiyo iliyoanza siku ya Jumamosi na kumalizika Jumatatu tarehe 18 Juni imewashirikisha wanawake kutoka pembe tofauti za mji huo.
Katika semina hiyo Bi Zainab Jumua mmoja wa wanafunzi waliohitimu masomo yao katika chuo cha masomo ya kidini cha Zahra (as) katika mji mtakatifu wa Qum nchini Iran na ambaye ni mwalimu katika Madrasa ya Darul Huda nchini Tanzania alizungumzia fadhila za kiakhlaqi, maisha na nafasi muhimu na tukufu ya Bibi Fatma (as) katika Uislamu. 1033558
captcha