IQNA

Maadhimisho ya kuzaliwa Imam wa Zama (af) kufanyika Uganda

17:31 - June 30, 2012
Habari ID: 2357578
Waislamu wa madhehebu ya Shia wakazi wa Jinja mji wa pili kwa ukubwa nchini Uganda, wanapanga kufanya maadhimisho makubwa ya kuzaliwa Imam wa Zama Imam Mahdi (af) mjini humo hapo Alkhamisi tarehe Tano Julai.
Maadhimisho hayo ambayo yamepangwa kuanza saa nne mchana kwa wakati wa Uganda na kumalizika kabla ya swala ya adhuhuri yatahudhuriwa na idadi kubwa ya wasomi, wanafikra na wapenzi wa Watu wa Nyumba ya Mtume (saw).
Sheikh Suleiman Imam wa Msikiti wa Mashia wa Jinja aliyehitimu masomo yake katika chuo cha kidini cha Jamiatul Mustafa (saw) al-Alamiya nchini Iran anatarajiwa kuzungumza katika maadhimisho hayo kuhusiana na ghaiba ya muda mrefu ya Imam Mahdi (af) na majukumu ya Mashia katika kipindi hiki muhimu. 1041138
captcha