IQNA

Mjumuiko Mkubwa wa 13 Aban mjini Tehran

IQNA - Makumi kwa maelfu ya watu walikusanyika mbele ya (Pango la Ujasusi) ubalozi wa zamani wa Marekani katikati mwa jiji la Tehran mnamo Novemba 3, 2024, kuadhimisha kumbukumbu ya kutwaliwa kwake, inayojulikana zaidi nchini Iran kama Siku ya Kitaifa ya Wanafunzi na Siku ya Kitaifa ya Mapambano dhidi ya Uistikbari au Ubeberu Ulimwenguni.

Miaka 46 iliyopita  yaani tarehe 13 Aban mwaka 1357 Hijria Shamsia  (sawa na Novemba 4, 1979), kulifanyika maandamano makubwa ya wanafunzi na wanachuo mjini Tehran, kulalamikia njama kadhaa wa kadhaa zilizokuwa zikifanywa na Marekani dhidi ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran.