Moja ya maeneo hayo ni ufa mwembamba ndani ya mlima, mahali ambapo Mtume Muhammad (SAW) alijificha kutafuta hifadhi baada ya kujeruhiwa katika vita hivyo.
Eneo la pili ni Msikiti wa Fasah, ambao unasadikiwa kuwa ni mahali alipokuwa akiendesha Swala baada ya kumalizika kwa vita hivyo.
Msikiti huu, ambao hivi karibuni umefanyiwa ukarabati, pamoja na ufa wa mlima huo, sasa ni maeneo maarufu yanayovutia wageni kwa sababu za kidini na kiutamaduni, wakiwemo Waislamu kutoka sehemu mbalimbali duniani wanaokuja kufanya ziara ya kiroho na kukumbuka historia tukufu ya Mtume na Maswahaba zake.