IQNA

Saudia yasitisha safari zote za ndege za kimataifa kutokana na hofu ya corona

15:38 - March 14, 2020
Habari ID: 3472565
TEHRAN (IQNA) – Saudi Arabia imesitisha safari zote za ndege za kimataifa kwa muda wa wiki mbili kuanzia Machi 15 ili kueneza ugonjwa wa COVID-19 maarufu kama kirusi corona.

Taarifa hiyo imesema raia wa Saudia na wakaazi wa kigeni nchini humo ambao walikuwa wamesafiri nje ya nchi na hawataweza kurejea kazini kutokana na marufuku hiyo watahesbiwa kuwa wako kwenye likizo rasmi. Aidha wakati wakirejea na kuwekwa kwenye karantini watahesabiwa kuwa pia wake kwenye likizo rasmi.

Hadi sasa Saudia imesema ina kesi 86 za walioambukizwa corona huku idadi hiyo ikiendelea kuongezeka.

3885144

captcha