Taarifa hiyo imesema raia wa Saudia na wakaazi wa kigeni nchini humo ambao walikuwa wamesafiri nje ya nchi na hawataweza kurejea kazini kutokana na marufuku hiyo watahesbiwa kuwa wako kwenye likizo rasmi. Aidha wakati wakirejea na kuwekwa kwenye karantini watahesabiwa kuwa pia wake kwenye likizo rasmi.
Hadi sasa Saudia imesema ina kesi 86 za walioambukizwa corona huku idadi hiyo ikiendelea kuongezeka.