IQNA

Imam wa Ijumaa wa Najaf:

Ashura, siku ya kimataifa ya kupambana na ugaidi

14:27 - December 18, 2010
Habari ID: 2049050
Imam wa swala ya Ijumaa ya mji mtakatifu wa Najaf Sayyid Sadruddin al Qubanchi amewataka walimwengu waitangaze siku ya tarehe 10 Muharram kuwa siku ya kimataifa ya mapinduzi ya walimwengu wote dhidi ya dhulma na aina zote za ugaidi.
Sayyid al Qubanchi ambaye alikuwa akihutubia waumini katika swala ya Ijumaa amesema kuwa katika siku ya Ashura yaani tarehe 10 Muharram, Waislamu hutangaza tena utiifu wao kwa malengo ya harakati na njia ya Imam Hussein (as).
Ameongeza kuwa kila mtu anayetaka izza, heshima, uhuru na kutokomezwa utawala wa Kizayuni wa Israel anapaswa kuhuisha jina la Imam Hussein kwani jina na wito wa mtukufu huyo umekomboa mataifa mbalimbali.
Imam wa swala ya Ijumaa ya Najaf pia amelaani mashambulizi ya kigaidi yaliyowalenga waombolezaji wa mauaji ya Imam Hussein (as) katika miji ya Baghdad na Diali huko Iraq na Chabahar nchini Iran.
Vilevile amewashukuru Waislamu katika nchi mbalimbali duniani kwa kushiriki kwa wingi katika shughuli za maombolezo ya tukio chungu la kuuawa mjukuu wa Mtume Muhammad (saw) Imam Hussein (as). 713547

captcha