IQNA

Ombi la Waziri wa Biashiara wa Sweden

8:19 - December 01, 2008
Habari ID: 1714343
Waziri wa Biashara wa Sweden ametaka kuimarishwa mazungumzo na ushirikiano wa nchi za Kiislamu na Umoja wa Nchi za Ulaya.
Gazeti la Arab News limeandika kuwa, Ewa Björling, Waziri wa Biashara wa Sweden ametoa pendekezo hilo katika mazungumzo yake na Zedhal Aliridha, waziri mwenzake wa Saudi Arabia na kuongeza kuwa kuimarishwa kwa uhusiano wa nchi za Kiislamu na Umoja wa Ulaya kutasaidia kurekebisha sura mbaya na potofu ya wazungu kuhusiana na Uislamu na Waislamu. Katika kuendelea na mazungumzo hayo, waziri huyo amesema kuwa picha waliyonayo watu wa Ulaya kuhusiana na ulimwengu wa Kiislamu si sahihi hata kidogo na kwamba, kuongezeka kwa mazungumzo kati ya pande mbili hizi yanaweza kusaidia sana kurekebisha jambo hilo, Mazungumzo hayo yalifanyika Jumamosi kati ya nchi hizo katika Ofisi ya Kibiashara ya Saudi Arabia huko mjini Jeddah kwa ajili ya kuongeza kiwango cha miamala ya nchi hizo katika nyanja za kibiashara. 327826
captcha