Gazeti la Shabiba la Oman limeandika kuwa mashindano hayo ya siku mbili yanasimamiwa na ofisi inayoshughulikia masuala ya wanafunzi wa vyuo vikuu katika maeneo mbalimbali ya Oman.
Washiriki katika mashindano hayo wanatakiwa kuwa wamehifadhi juzuu za 9, 10, 11, 12 za Qur'ani Tukufu na haditi 30 za Mtume (saw) na kuwa na uwezo wa kuzitolea sherhe na ufafanuzi.
Miongoni mwa malengo ya mashindano hayo ni kuzidisha maarifa ya Qur'ani ya wanafunzi wa vyuo vikuu na kueneza moyo wa ushindani sahihi kati yao.
Washiriki katika mashindano hayo walishinda mashindano ya awali ndani ya vyuo vikuu na kufanikiwa kuingia duru ya mwisho itakayofanyika Alkhamisi ijayo. 370811