Mussa Salman Yasin amesema kuwa kaburi la Nabii Yahya (as) limegunduliwa katika bonde la kale linayojulikana hadi sasa kwa jina la Mar Yahya katika eneo la kaskazini mashariki mwa Tulini huko kusini mwa Lebanon.
Mtafiti huyo amesema kuwa eneo hilo linaungana na eneo la Qabrikha la kusini mwa Lebanon na kwa mujibu wa riwaya mashuhuri Nabii Yahya bin Zakaria (as) alikatwa kichwa na mfalme muovu wa Roma Herod katika eneo hilo.
Mussa Salman Yasin amesema kuwa bonde la Mar Yahya lina turathi nyingi za thamani za kihistoria na kidini na kwamba historia inaonyesha kuwa kuna zaidi ya athari 50 za Mitume wa Mwenyezi Mungu na watoto wao katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa kisa cha Nabii Yahya bin Zakaria kilichotajwa kwenye vitabu vya kidini na kihistoria, Mtume huyo wa Mwenyezi Mungu aliuawa kwa kukatwa kichwa na mfalme wa Roma. 390215