IQNA

Kongamano la Kimataifa la "Uislamu na Uhusiano wa Kimataifa" kufanyika Gilan, Iran

17:49 - September 08, 2010
Habari ID: 1990591
Kongamano la Kimataifa la "Uislamu na Uhusiano wa Kimataifa" litafanyika Machi mosi na pili mwakani katika Chuo Kukuu cha Gilan kaskazini mwa Iran.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, kongamano hilo litafanyika kwa himaya ya Jumuiya ya Kielimu ya Uhusiano wa Kimataifa, Wizara ya Sayansi, Utafiti na Teknolojia, Wizara ya Mambo ya Nje, Wizara ya Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu, Chuo Kikuu cha Imam Sadiq (AS), Chuo Kikuu cha Allamah Tabatabai, Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Azad Kitengo cha Rasht na Mkuu wa Mkoa wa Gilan.
Kongamano hilo linatazamiwa kujadili masuala kama vile mielekeo ya siasa za kimataifa, fiqhi ya Kiislamu na siasa za kimataifa, Uislamu na siasa na muundo wa kimataifa, mustakbali wa harakati za Kiislamu katika mfumo wa Kimataifa n.k.
651242
captcha