IQNA

Mashindano ya kwanza ya kitaifa ya Qur'ani kwa wanawake wa Iraq

11:35 - October 02, 2010
Habari ID: 2005202
Duru ya kwanza ya mashindano ya kitaifa ya Qur'ani kwa wanawake wa Iraq imepangwa kufanyika katika mji mtakatifu wa Kadhimein.
Mashindano hayo ambayo yameandaliwa na Taasisi ya Qur'ani ya al-Iraqiyyah yamepangwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu wa Oktoba. Rafi' al-Aamiri, Mkuu wa taasisi hiyo iliyo na makao makuu yake mjini Kadhimein amesema kuhusu suala hilo kwamba, wanawake walio na hamu ya kushiriki kwenye mashindano hayo wanaweza kufika kwenye makao hayo na kusajili majina yao kuanzia saa tisa hadi kumi na mbili jioni kwa wakati wa Iraq.
Amesema mtihani wa utangulizi utafanyiwa watu watakaosajili majina yao na kwamba iwapo watapata alama zinazohitajika, wataruhusiwa kushiriki katika hatua ya pili na ya mwisho ya mashindano hayo. 666484
captcha