Akirejelea ujumbe wa kihistoria kuhusu tukio la Ghadir Khum ambalo amekumbusha kuwa linakubaliwa na madhehebu ya Kishia na Kisuni, Ayatullah Kashani amewataka Waislamu duniani kujenga msingi wa mshikamano ambao utakuwa ngao ya kujilinda dhidi ya uadui na uhasama unaofanywa na maadui wa Uislamu.
Khatibu wa swala ya Ijumaa wa mjini Tehran ameashiria umuhimu wa kupatikana umoja katika ulimwengu wa Kiislamu ili kukomesha uadui na mizozo inayochochewa na Magharibi katika nchi za Iraq, Afghanistan, Lebanon na Palestina na kongeza kuwa, kumtegemea Allah, kutekeleza wajibu na kusimamia haki na ukweli ndiko kutakakoufanya ulimwengu wa Kiislamu kupiga hatua na kufaulu katika vita hivyo dhidi ya maadui wake.
Aidha, Ayatullah Kashani amelipongeza Jeshi la Kujitolea la Basiji la Iran kwa kujitolea muhanga na kuhakikisha Mapinduzi ya Kiislamu hayayumbi.
701627