Ripoti zinasema kuwa maelfu ya waombolezaji wanatembea kwa miguu wakielekea mjini Najaf kwa ajili ya kuumbuka tukio chungu la kufariki dunia Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) licha ya baridi kali.
Vilevile wananchi wa Iraq wameweka mahema kandokando ya barabara hizo ambayo yanatoa huduma za vyakula, maji, na tiba kwa maelfu ya watu wanaokwenda kuzuru kaburi la Imam Ali (as) na kuhudhuria marasimu ya maombolezo ya kifo cha Mtume Muhammad (saw).
Katika upande mwingine Idara ya Afya ya mji mtakatifu wa Najaf imeanzisha vituo zaidi ya 20 vya afya kwa ajili ya kutoa huduma kwa wanaofanya ziara mjini humo. 740391