IQNA

Saudia yawazuia maqari wa Iran katika mashindano ya Qur'ani

9:10 - March 15, 2011
Habari ID: 2095985
Maqari wa Qur'ani kutoka Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wameshindwa kushiriki katika Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Majeshi ya Nchi za Kiislamu huko Saudi Arabia baada ya kunyimwa visa.
Kwa mujibu wa kapteni Mehdi Meydani Naibu Mkuu wa Kituo cha Darul Qur'an katika Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema serikali ya Saudi Arabia haikutoa visa kwa washiriki Wairani na hivyo hawajaweza kushiriki katika mashindano hayo ya Qur'ani.
Ameongeza kuwa juhudi kubwa zilifanywa na maafisa wa Iran kutatua tatizo hilo lakini hawakufanikiwa.
Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Majeshi ya Nchi za Kiislamu yalianza Machi 13 katika mji mtakatifu wa Makka na yataendelea hadi Machi 25. Nchi 16 zinashiriki katika mashindano hayo.
762479
captcha