IQNA

Hatua ya pili ya mashindano ya kimataifa ya Qur'ani kwa watoto yaanza Qatar

17:45 - April 05, 2011
Habari ID: 2101151
Hatua ya pili ya mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu kwa watoto, ambayo yameandaliwa na televisheni ya watoto ya al-Jazeera kwa ushirikiano wa Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Qatar yalianza nchini humo hapo jana Jumatatu tarehe 4 Aprili.
Mashindano hayo yanafanyika ili kuwachagua washindi watakaoshiriki katika hatua ya mwisho ya mashindano hayo ambayo imepangwa kufanyika katika mwezi mtukufu wa Ramadhani. Walio na hamu ya kushiriki katika mashindano hayo wanaweza kuandikisha majina yao kupitia mtandao wa televisheni ya al-Jazeera ya watoto, mashindano ambayo kwa mara ya kwanza kabisa yanawashirikisha watoto Waislamu wa kiume na kike kutoka pembe zote za dunia. Watoto 63 tu ndio watakaochaguliwa kutoka kwenye hatua hiyo ili kushindana katika hatua ya mwisho ya mashindano hayo ambapo washindi wanne wa mwisho watapata zawadi ya kuchukua nafasi ya kwanza. 769215
captcha