IQNA

Kitabu cha 'Wanawake wenye imani Katika Qurani na Maisha' chachapishwa

13:47 - April 17, 2011
Habari ID: 2107105
Kitabu chenye anuani ya "Wanawake wenye imani katika Qurani na Maisha' (“Kur’an-Hayat Ekseninde Mümin Kadın” ) kimechapishwa nchini Uturuki na shirika la uchapishaji la EKIN.
Kati ya mada zilizojadiliwa katika kitabu hicho chenye kurasa 200 ni, 'Lugha ya Qurani na Wanawake', 'tafauti za wanawake na wanaume' na 'ushirikiano wa wanaume na wanawake.
Mada zingine ni 'Wanawake wenye imani katika maisha ya kijamii', 'Qurani na Mwanamke', 'aya za Qurani kuhusu wanawake' , 'ndoa', 'jukumu la wanaume' na 'mwanamke kumtii mume wake'.
Aidha kitabu hicho kimejadilia maudhui ya 'Wanawake katika Harakati za Kiislamu'.
Mwandishi wa kitabu hiki ni afisa wa Jumuiya ya Uhuru wa Maoni na Haki za Kielimu nchini Uturuki.
775137
captcha