IQNA

‘Nafasi ya Vyombo vya Habari katika kutetea Qur’ani’

13:37 - June 11, 2011
Habari ID: 2135602
Kongamano la ‘Nafasi ya Vyombo vya Habari katika Kutetea Heshima ya Qur’ani limefanyika Juni 9 katika mji mkuu wa Iraq, Baghdad.
Kongamano hilo limeandaliwa na Chuo Kikuu cha An Naharin chini ya usimamizi wa Kamati ya Mwaka wa Kutetea Qur’ani. Kongamano hilo limedhuhuriwa na viongozi wa kidini, wabunge pamoja na washika dau katika sekta za habari na utamaduni.
Aidha wawakilishi wa ofisi ya Sayyid Muhammad Baqer Sadr walihudhuria kikao hicho.
Kufuatia hatua ya mhubiri Mkristo Mmarekani ya kuichoma moto Qur’ani Tukufu mwezi Machi, Bunge la Iraq limeutangaza mwaka huu kuwa ‘Mwaka wa Kuitetea Qur’ani Tukufu’
805941
captcha