IQNA

Mkuu wa Baraza la Wahubiri wa Kiislamu Ivory Coast ateuliwa

15:32 - July 19, 2011
Habari ID: 2156396
Baraza la Wahubiri wa Kiislamu Ivory Coast limemteua Sheikh Sadiq Sizeh kuwa mwenyekiti wake mpya.
Katika uchaguzi uliofanyika Julai 18, baraza hilo lenye wanachama 35 kutoka madhehebu mbalimbali ya Kiislamu lilimchagua kiongozi mpya baada ya muhula wa Sheikh Bubakar Kulibali kumalizika.
Mwenyekiti mpya wa baraza hilo amesema: “Mikutano yetu ni fursa ya kujadili masuala ya Kiislamu na matatizo ya jamii ya Kiislamu. Hii ni katika hali ambayo tunafungamana na kufanya kila tuwezalo kuimarisha umoja wa Waislamu na kujiepusha na mifarakano ya kidini”.
Amesema baraza hilo litazingatia zaidi suala la madrasa za Qur’ani na kuandaa mipango ya kuwasaidia wanafunzi wanaohitimu kutoka madrasa hizo.
827639
captcha