Hayo ni kwa mujibu wa Masood Nikdast, karii maarufu wa Qur’ani nchini Iran ambaye ameongeza kuwa maonyesho hayo ni tukio kubwa ambalo huwalkutanisha pamoja wasomi na wanaharakati wa Qur’ani kitaifa na kimataifa.
Amepongeza mafanikio yaliyopatikana hapa nchini katika uga wa Qur’ani ambayo yamewasilishwa katika maonyesho hayo na kusema taasisi zaidi za Qur’ani nchini zihusishwe. Amesema kuna vipawa tele vya Qur’ani katika miji mbalimbali ya Iran.
830749