Kozi hiyo inajumuisha mafunzo kuhusu lugha ya Qur’ani, tadaburi juu ya aya za Qur’ani, Nahjul Balagha, mbinu za kufundisha, nahau ya Kiarabu na kufunza Qur’ani Tukufu kwa Kiingereza.
Wale watakaohudhuria kozi hiyo na kufanikiwa watapewa vyeti.
Kozi hiyo imeandaliwa ili kutoa fursa kwa washiriki kuhifadhi Qur’ani. Kusoma aya za Qur’ani, kuimarisha ufahamu wa Qur’ani na lugha ya Kiarabu.
Maonyesho ya 19 ya Kimataifa ya Qur’ani yanaendelea katika Uwanja wa Sala wa Imam Khomeini RA mjini Tehran kila siku kuanzia saa 11 jioni hadi saa sita usiku hadi tarehe 26 Ramadhani.
836331