IQNA

Filamu ya visa vya shakhsia wa Qura'ni yaanza kutengenezwa Misri

15:46 - October 31, 2011
Habari ID: 2215204
Filamu inayozungumzia visa 11 vya shakhsia mbalimbali katika Qur'ani Tukufu itaanza kutengenezwa nchini Misri tarehe 15 Novemba.
Kwa mujibu wa gazeti la al-Ahram linalochapishwa Misri, filamu hiyo itatengenezwa na Yahya al-Fakhrani, msanii mashuhuri wa Misri ambaye huko nyuma pia alitengeneza filamu nyingine ya visa vya wanyama katika Qur'ani.
Baadhi ya visa ambavyo tayari vimechaguliwa kwa jili ya kutengeneza filamu hiyo ni pamoja na As'habul Ukhdud, Nabii Musa na Hadhrat Khidhr (as), Talut na Jalut, Watu wa Peponi, Hakimu Luqman, Qarun na Dhul Qarnein.
Al-Fakhrani amesema kuwa amechukua uamuzi wa kutengeneza filamu hiyo baada ya kupokelewa vyema filamu yake ya kwanza iliyohusiana na visa vya wanyama kwenye Qur'ani Tukufu ambayo ilionyeshwa katika kipindi cha mwezi mtukufu uliopita wa Ramadhini.
Mwandishi wa filamu hiyo Ahmad Bahjat amesema kuwa tayari sehemu 15 za filamu hiyo zimewekwa tayari kwa ajili ya upigaji picha. 890459
captcha