IQNA

Wizara ya Tunisia yalaani shambulio la Mawahabi katika maeneo matakatifu

17:42 - May 15, 2012
Habari ID: 2326730
Wizara ya Utamaduni ya Tunisia jana Jumatatu ilitoa taarifa ikilaani shambulio lililofanywa hivi karibuni na makundi ya Kiwahabi katika maeneo matakatifu yanayozuriwa na waumini wa Kiislamu katika miji tofauti ya nchi hiyo.
Kwa mujibu wa tovuti ya lacote, wizara hiyo imesisitiza kwamba maeneo hayo matakatifu ni sehemu ya turathi na utajiri wa kiutamaduni wa Tunisia na kulaani vikali hujuma dhidi ya maeneo hayo ya ibada. Huku akilaani vikali kitendo hicho Mahdi Mabrouk, Waziri wa Utamaduni wa Tunisia ametoa pendekezo la kubuniwa kamati maalumu itakayosimamia na kuchunga turathi na maeneo matakatifu kama hayo dhidi ya hujuma za watu waovu. Wakati huohuo, wizara yake imetangaza kwamba askari usalama wa nchi hiyo wanachunguza na kufuatilia watu waliohusika na hujuma hiyo. Vyombo vya habari vya nchi hiyo vimeashiria itikadi potofu za makundi ya Mawahabi kuhusiana na ziara katika maeneo matakatifu na kusema kuwa ndiyo yamekuwa yakiwachochea wafuasi wao kuharibu maeneo hayo.1008325
captcha