IQNA

Mashindano ya Qur'ani kutangazwa moja kwa moja kupitia redio nchini Ufaransa

12:59 - July 04, 2012
Habari ID: 2360973
Duru ya kwanza ya mashindano ya Qur'ani Tukufu nchini Ufaransa yatatangazwa moja kwa moja kupitia redio Pastel FM.
Kwa mujibu wa tovuti ya Safirnews, mashindano hayo ya kiraa ya Qur'ani Tukufu ambayo yatafanyika katika mwezi mtukufu wa Ramadhani yatawahusisha vijana wa miaka 8 hadi 26.
Duru za utangulizi za mashindano hayo ambayo yamepangwa kufanyika tarehe 12, 13 na 14 za mwezi huu wa Julai kabla ya washindi kushiriki katika mashindano ya mwisho yaliyopangwa kufanyika tarehe 17 Agosti.
Watu walio na hamu ya kushiriki katika mashindano hayo wana fursa ya hadi kufikia tarehe 10 Julai kusajili majina yao kupitia mtandao wa intaneti. Washindi wa mashindano hayo watatunukiwa zawadi nono ikiwemo ya kuhiji mjini Makka Saudi Arabia. 1044766
captcha