Hayo yametangazwa na Mkuu wa Masuala ya Utamaduni katika Shirika la Wakfu mkoani Kermanshah Sheikh Mohsen Suleimani ambaye ameongeza kuwa vikao hivyo vya Qur’ani vitafanyika katika misikiti na maeneo matakatifu mkoani humo.
‘Mwezi mtukufu wa Ramadhani ni fursa nzuri kwa wale wanaotaka kujikurubisha zaidi na Qur’ani Tukufu,’ ameongeza.
Katika upande mwingine maqarii wa Iran wameelekea katika nchi mbalimbali duniani kushiriki katika vikao vya Qur’ani katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.
1048781