IQNA

Shirika la Habari la Qur'ani ni rasilimali muhimu ya Iran ya Kiislamu

17:53 - July 24, 2012
Habari ID: 2376137
Waziri wa Utamaduni na Muongozo wa Kiislamu wa Iran amepongeza Shirika la Kimataifa la Habari za Qur'ani IQNA kwa utendaji wake bora na kulitaja shirika hili kuwa ni rasilimali kubwa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Akizungumza alipotemebela kibanda cha IQNA katika Maonyesho ya 20 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Tehran, Seyyid Muhammad Husseini amepongeza IQNA kwa kuongeza idadi ya lugha zake hadi 40.
Huku akiwashukuru waandishi wa IQNA kwa juhudi zao, amewataka kuzidisha harakati zao kwa raghba kubwa zaidi ya huko nyuma.
Amesema ili kuwa na jamii bora, kuna haja ya kusambaza habari kuhusu harakati za Qur'ani.
Aidha ameyataja Maonyesho ya Kimataifa ya Qur'ani kuwa tukio kubwa ambalo halina mfano wake duniani.
Maonyesho hayo ya mwezi moja yanatazamiwa kuendelea hadi tarehe 25 ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
1059846
captcha