IQNA

Ujumbe wa makari wa Misri watembelea Taasisi ya Darul Qur'anil Karim mjini Tehran

17:11 - July 24, 2012
Habari ID: 2376360
Ujumbe wa makari na mahafidh 77 kutoka nchini Misri ambao uko hapa nchini kwa mwaliko wa Idara ya Masuala ya Qur'ani Tukufu na Maarifa ya Kidini ya Taasisi ya Utamaduni na Mawasiliano ya Kiislamu umetembelea taasisi ya Darul Qur'anil Karim.
Akizungumza katika hafla hiyo, Muhammad Ridha Sulhju, mwanachama wa bodi ya wasimamizi wa Darul Qur'anil Karim amesema kwamba Wairani wana uzoefu wa miaka 50 wa kunufaika na mbinu za usomaji Qur'ani za Wamisri na kwamba kwa uchache Wairani wapatao 50 huwa wanasoma kwenye idhaa za taifa kwa mbinu hizo.
Amesema kwa baraka za Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran hivi sasa mafundisho ya usomaji Qur'ani, hifdhi na maarifa ya Qur'ani Tukufu yameenea katika pembe zote za nchi ambapo hii leo kuna mamia ya makari na mahafidh wa Qur'ani katika kila mji na kijiji nchini Iran.
Baada ya kutolewa hutoba za kuukaribisha ujumbe huo, ujumbe huo ulitemebelea sehemu na vitengo tofauti vya Darul Qur'anil Karim ambayo hujishughulisha na masuala mbalimali ya uchapishaji, usahihishaji, tathmini na usimamiaji wa masuala ya kitabu hicho kitakatifu.1060948
captcha