IQNA

Nakala za kale za Qur'ani zagunduliwa Uturuki

22:31 - January 30, 2013
Habari ID: 2488822
Maafisa wa serikali ya Uturuki wametangaza kuwa wamegundua nakala kadhaa za kale za kitabu kitakatifu cha Qur'ani zilizoandikwa kwa hati za mkono katika msikiti mmoja ulioko katika mji wa Qaunia katika jimbo la Anatoly.
Nakala hizo za kale za Qur'ani zimegunduliwa katika msikiti wa wilaya ya Qaunia na inakadiriwa kuwa zina umri wa zaidi ya miaka 200.
Nakala hizo za Qur'ani ambazo zimeandikwa miaka 200 hadi 250 iliyopita zimegunduliwa wakati wa kufanya usafi kwenye paa la msikiti na maktaba yenye turathi za maandishi ya hati za mkono.
Mkuu wa maktaba ya Qaunia amesema kuwa nakala hizo 32 za Qur'ani zitakarabatiwa katika kipindi cha mwaka mmoja na kuoneshwa wka watu wote.
amesema hii si mara ya kwanza kugundyliwa nakala za kale za Qur'ani katika eneo hilo.1180206
captcha