Mawakili wa zaidi ya wafungwa 10 wa jela hiyo walitangaza jana kuwa mgomo huo unafanyika kupinga upekuzi mpya unayofanywa na askari wa Marekani dhidi ya wafungwa hao ikiwa ni pamoja na kukivunjia heshima kitabu kitukufu cha Qur'ani.
Wakili wa raia wa Yemen Qalib al Baihani anayeshikiliwa huko Guantanamo amesema kuwa mteja wake pamoja na wafungwa wengine kadhaa wamesema kuwa wenzao wote wanaoshikiliwa katika kambi nambari sita wamo katika mgomo wa kula.
Mawakili wa wafungwa hao wanasema wamemwandikia barua kamanda wa kambi ya Guantanamo wakimpasha habari ya hali mbaya ya wafungwa hao. Wamesema kuwa wamemweleza pia kuhusu vitendo vya askari magereza wa Marekani vya kukivunjia heshima kitabu kitukufu cha Qur'ani. 1203123