IQNA

Awamu ya kwanza mashindano ya Qur'ani Kuwait yamalizika

19:23 - March 25, 2013
Habari ID: 2513400
Awamu ya kwanza ya mashindano ya 16 ya kitaifa ya Qur'ani nchini Kuwait imemalizika.
Mkurugenzi wa Baitul Qur'ani ya Kuwait, Nasir al Dabbus ambaye ndiye mwenyekiti wa mashindano hayo amesema kuwa awamu ya kwanza ya mashindano hayo imemalizika na kwamba tume ya mashindano hayo itaanza kuwasiliana na washiriki wa awamu ya mwisho.
Nasir al Dabbus amesema kuwa, mashindano hayo yanafanyika katika vitengo vinne vya watoto wadogo, mabarobaro, vijana na watu wazima. Ameongeza kuwa mwaka huu kitengo cha watu wazima kinawashirikisha raia wa Kuwait na wa nchi za nje wanaoishi nchini humo.
Amesema kuwa awamu ya kwanza ya mashindano hayo ya Qur'ani lifanyika katika mikoa sita ya Kuwait na kwamba kamati 24 zilizimamia mashindano hayo.
Amesema raia wa nchi 46 wanaoishi Kuwait wameshiriki katika awamu ya kwanza na kwamba idadi ya washiriki imeongezeka ikilinganishwa na miaka iliyopita. 1205972
captcha