Maonyesho hayo yalizinduliwa Jumatano, yakikaribishwa zaidi ya wachapishaji 2,500 wa Iran na 60 wa kigeni ambao wamewasilisha vitabu vyao vipya zaidi katika hafla hiyo.
Duru ya pili ya uchaguzi wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (bunge la Iran) pia ulifanyika siku ya Ijumaa na kulikuwa na kituo cha kupigia kura kwenye maonyesho hayo ya vitabu.
Yakiendeshwa chini ya kauli mbiu "Tusome na Tuunde," Maonyesho ya 35 ya Kimataifa ya Vitabu ya Tehran yataendelea hadi Mei 18 jijini Tehran katika Eneo la Sala (Musalla) la Imam Khomeini.