IQNA

Vituo vya Qur’ani Tehran vyaanza tena masomo ya ana kwa ana

22:21 - November 17, 2021
Habari ID: 3474570
TEHRAN (IQNA)- Vituo vya Masomo ya Qur’ani vya Baraza la Jiji la Tehran vitaanza tena masomo ya ana kwa ana baada ya kufungwa kwa muda mrefu kutokana na janga la COVID-19.

Hayo yamedokezwa na Sayyid Hossein Mousavi Baladeh, mkuu wa masuala ya Qur’ani katika Baraza la Jiji la Tehran katika mahojiano na IQNA.

Ameongeza kuwa, kufuatia kulegezwa sheria za kuzuia kuenea COVID-19 baada ya maambukizi kupungua, hvi sasa Vituo vya Masomo ya Qur’ani sasa vitaanza masomo kwa kuhudhuria wanafunzi na waalumu ana kwa ana.

Amesema hivi sasa kuna taasisi 11 za Darul Qur’an ambazo zinafungamana na Baraza la Jiji la Tehran ambapo mbali na kutoa mafunzo kwa umma pia hutumika kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa baraza hilo.

Aidha ameelezea matumaini kuwa bajeti ya vituo vya Qur’ani itaongezwa ili kustawisha zaidi harakati za Qur’ani katika mji mkuu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

4009801

captcha