waislamu - Ukurasa 104

IQNA

Zaidi ya Waislamu 1,000 wametimuliwa katika mji wa Bossangoa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati na kuelekea katika nchi jirani ya Chad huku kukiwa na hofu ya kuuawa kwa umati Waislamu mikononi mwa wanamgambo wa Kikristo.
Habari ID: 1395037   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/04/14

Kundi lenye misimamo mikali ya Kikristo la Anti Balaka sasa limeanza kutumia mbinu mpya kwa ajili ya kuua Waislamu katika Jamhuri ya Afrika ya Kati kwa kuwauzia vyakula vyenye sumu. Hadi sasa makumi ya watoto wadogo wameripotiwa kufariki dunia katika mji wa Buda kutokana na mbinu hiyo ya mauaji.
Habari ID: 1392667   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/04/09

Huku katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban ki Moon akielezea wasi wasi wake kuhusu kuendelea kukandamizwa Waislamu Jamhuri ya Afrika ya Kati, Shirika la Kuwahudumi wakimbi la umoja huo, UNHCR Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wakimbizi UNHCR limetangaza kuwa liko tayari kuwahamishia sehemu salama Waislamu wa nchi hiyo.
Habari ID: 1390350   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/04/03

Taarifa zimeeleza kuwa Waislamu katika moja ya miji ya Jamhuri ya Afrika ya Kati wametishiwa kuuawa.
Habari ID: 1389972   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/03/30

Baraza la Mahusiano ya Kiislamu nchini Marekani (CAIR) limelalamikia hatua ya banki moja ya nchi hiyo ya kuzifunga akaunti za fedha za Waislamu. Baraza la Mahusiano ya Kiislamu la Marekani sambamba na kulalamikia hatua hiyo ya Tawi la Banki ya Minessota limewataka maafisa wa benki hiyo kutoa maelezo kuhusiana na hatua hiyo isiyokubalika.
Habari ID: 1384501   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/03/09

Afisa mwandamizi wa Umoja wa Mataifa amesema karibu Waislamu wote waliokuwa wakiishi mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bangui, wamelazimika kuondoka mjini humo kutokana na jinai za magaidi wa Kiksristo.
Habari ID: 1384500   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/03/09

Mbunge mmoja wa Chad amesisitiza kuhusu ulazima wa kutuma askari wa kimataifa kulinda maisha ya Waislamu Jamhuri ya Afrika ya Kati. Mohammad Ibn Zain ameongeza kuwa kuendelea mauaji ya umati ya Waislamu huko Jamhuri ya Afrika ya Kati ni natija ya kimya cha jamii ya kimataifa.
Habari ID: 1379190   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/02/24