Mahujaji takribani milioni tatu wa Nyumba Tukufu ya Allah SWT leo Ijumaa wameanza kutekeleza ibada ya Hijja, ambapo jana usiku walianza kukusanyika katika viwanja vya Arafa nje ya mji mtukufu wa Makka.
Habari ID: 1456586 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/03
Mashindano ya Qur’ani yamefanyika nchini Rwanda chini ya himya ya Jumuiya ya Waislamu nchini humo.
Habari ID: 1455972 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/30
Mahakama moja ya Kenya imetoa uamuzi wa kupiga marufuku vazi la Hijabu katika shule moja nchini humo jambo ambalo limewakasirisha sana Waislamu wakiwemo wazazi na wanazuoni wa Kiislamu ambao wameitaja hukumu hiyo kuwa ni hatua nyuma katika uhuru wa kuabudu nchini humo.
Habari ID: 1455483 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/29
Wanazuoni waandamizi wa Kishia na Kisunni nchini Uingereza wamefanya kikao cha pamoja na kujadili njia za kuimarisha umoja miongoni mwa Waislamu sambamba na kukabiliana na kampeni za kuibua fitina katika ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 1449625 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/14
Rais Hassan Rouhani
Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sawa na siku za huko nyuma itatumia uwezo wake wote kwa ajili ya kuukomboa mji wa Quds na Msikiti wa Al Aqsa ambao ni kibla cha kwanza cha Waislamu sambamba na kulisaidia taifal linalodhulumiwa la Palestina.
Habari ID: 1445555 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/01
Mufti Mkuu wa Bulgaria ametahadharisha juu ya kuongezeka mashambulio yaliyoratibiwa dhidi ya Waislamu na maeneo ya ibada ya Waislamu katika nchi hiyo ya Ulaya.
Habari ID: 1445545 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/01
Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar wangali wanaishi katika hali ngumu na mazingira mabaya na makumi ya maelfu miongoni mwao wanakabiliwa na uhaba wa chakula, maji na huduma za afya.
Habari ID: 1437511 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/08/09
Jumuiya ya Waislamu nchini Nigeria imelaani mauaji ya Waislamu wa Kishia yaliyotekelezwa katika siku ya kimataifa ya Quds. Kwa mujibu wa ripoti hiyo jumuiya hiyo imelaani mauaji hayo iliyoyataja kuwa ya kinyama.
Habari ID: 1434577 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/07/28
Taasisi ya Imam Hussein AS katika eneo la Bugiri Mashariki mwa Uganda ni moja ya vituo muhimu zaidi vya kuhubiri Uislamu na maarifa ya Ahul Bayt AS katika eneo hilo.
Habari ID: 1432798 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/07/23
Rais Hassan Rouhani
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema matatizo wanayokumbana nayo Waislamu hivi sasa ni matokeo ya kutoyazingatia mafundisho ya Qur'ani Tukufu.
Habari ID: 1428807 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/07/13
Mjumbe mwandamizi wa Kamati ya Afya ya Shirikisho la Soka Duniani FIFA amesema kuwa, wachezaji Waislamu watakaofunga mwezi mtukufu wa Ramadhani, hawataathirika kiafya wakati wa kuendelea michuano ya kombe la dunia nchini Brazil.
Habari ID: 1422159 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/06/24
Msemaji wa Jumuiya ya Waislamu katika Jamhuri ya Afrika ya Kati amesema, wanamgambo wa Kikristo nchini humo wamewaua vijana watatu Waislamu na kukatakata viungo vyao vya mwili.
Habari ID: 1412082 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/05/29
Tarehe 27 Rajab Mwaka wa Tembo na akiwa na umri wa miaka 40, Mtume Muhammad (SAW) alikuwa juu ya kilele cha Mlima Hira, akijishughulisha na ibada ndani ya pango la mlima huo, ambapo ghafla malaika Jibril AS alimteremkia huku akiwa amebeba wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu SW.
Habari ID: 1411465 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/05/27
Mwislamu aliyekuwa na umri wa miaka 65 amepoteza maisha baada ya kushambuliwa na polisi wa utawala wa Mabuddha nchini Myanmar.
Habari ID: 1402630 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/05/03
Katika vipindi mbali mbali vya historia, wanafikra wameweza kunawiri katika nyuga za utamaduni na sayansi na hivyo kuwafungulia wanaadamu wengi njia ya nuru na saada.
Habari ID: 1402070 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/05/02
Hali ya usalama katika mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bangui, inazidi kuwa mbaya huku vitendo vya mauaji dhidi ya Waislamu vikiendelea kuripotiwa.
Habari ID: 1398695 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/04/22
Askofu Mkuu wa zamani wa Kanisa la Anglikana nchini Afrika Kusini ametahadharisha juu ya kukaribia kutumbukia Jamhuri ya Afrika ya Kati kwenye mauaji ya kimbari.
Habari ID: 1398694 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/04/22
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, kuuletea madhara mshikamano na kuzusha mizozo baina ya Waislamu wa Kishia na Kisunni ni moja ya vithibitisho vya kukufuru neema za Mwenyezi Mungu.
Habari ID: 1397724 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/04/20
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC imelaani hatua mpya ya serikali ya Myanmar kuondoa jina jamii ya Waislamu wa Rohingya katika takwimu rasmi za nchi hiyo.
Habari ID: 1397232 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/04/19
Viongozi wa Kiislamu nchini Kenya wamewataka raia wa nchi hiyo kuwa na umoja na mshikamano. Viongozi hao wamekutaja kudumishwa umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi kuwa ni jambo muhimu la lenye udharura.
Habari ID: 1396701 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/04/19