IQNA

Mauaji ya Waislamu CAR, natija ya kimya cha jamii ya kimataifa

11:26 - February 24, 2014
Habari ID: 1379190
Mbunge mmoja wa Chad amesisitiza kuhusu ulazima wa kutuma askari wa kimataifa kulinda maisha ya Waislamu Jamhuri ya Afrika ya Kati. Mohammad Ibn Zain ameongeza kuwa kuendelea mauaji ya umati ya Waislamu huko Jamhuri ya Afrika ya Kati ni natija ya kimya cha jamii ya kimataifa.

Kwa mujibu wa  Shirika la Kimataifa la Habari za Qur'ani IQNA,Ban Ki-moon Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti za kukomesha mauaji na umwagikaji damu katika Jamhuri ya Afrika ya Kati. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewataka Waislamu na Wakristo nchini humo washirikiane  kwa minajili ya kuijenga nchi yao. Ban Ki moon ameitaka jamii ya kimataifa kushirikiana katika kupeleka misaada ya kibinadamu  Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Wakati huohuo, kundi la Anti Balaka limewashambulia na kuwaua Waislamu watatu  waliokuwa ndani ya gari ndogo ya abiria kwa kuwapiga risasi na kuwakatakata kwa visu na mapanga karibu na uwanja wa ndege wa Bangui.
Hivi karibuni shirika la kutetea haki za binaadamu Human Rights Watch lilitaka hatua za haraka zichukuliwe kwa lengo la kuzuia mauaji ya halaiki ya Waislamu huko Jamhuri ya Afrika ya Kati. Waislamu ni takribani asilimia 15 ya watu milioni 4.6 katika Jamhuri ya Afrika ya Kati. Ripoti zinasema kuwa magenge ya magaidi Wakristo wenye misimamo mikali wamewaua maelfu ya Waislamu nchini humo huku mamia ya maelfu wakilazimika kukimbilia katika nchi jirani. Kuna askari 1,600 wa  Ufaransa na maelfu ya askari wengine wa kulinda amani kutoka nchi za Kiafrika huko Jamhuri ya Afrika ya Kati lakini wameshindwa kuzuia mauaji ya Waislamu yanayofanywa na magaidi Wakristo.
1378500

Kishikizo: JAMHURI moon waislamu car
captcha