IQNA

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu

Njama za adui ni kuchochea vita kati ya Suni na Shia

10:31 - June 29, 2014
Habari ID: 1423568
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametahadharisha juu ya njama za adui za kuchochea mgogoro wa kidini kati ya Waislamu wa madhehebu ya Shia na Suni ili kuvuruga wimbi la mwamko wa Kiislamu.

Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema kwamba, adui anachochea vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Iraq na kuwapiganisha Shia na Suni ili kukabiliana na wimbi la  mwamko wa Kiislamu. Akizungumza Jumamosi hii, Ayatullah Khamenei aliashiria mgogoro unaoendelea nchini Iraq na kusema kuwa, mabaki ya utawala uliopinduliwa wa dikteta saddam Hussein na kundi la watu wajinga na majahili wanatekeleza jinai katika nchi hiyo. Aidha Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kwamba, kinachojiri nchini Iraq si vita kati ya Shia na Suni bali ni vita vya ugaidi na wanaounga mkono nchi za Magharibi dhidi ya wapinzani wa ugaidi na watetezi wa uhuru wa mataifa mbalimbali.  Ayatullah Ali Khamenei amesema hayo akihutubia familia za mashahidi waliopoteza maisha kwenye shambulio la bomu la kigaidi ulililotokea tarehe 7 Tir mwaka 1360 wa Kiirani  sawa na Juni 1981. Watu 72 wakiwemo mawaziri na wabunge 72 wa Iran walipoteza maisha katika mlipuko huo akiwemo Ayatullah Dakta Muhammad Beheshti aliyekuwa Mkuu wa Mahakama za Iran.

1423142

Kishikizo: khamenei
captcha