IQNA

Mkutano wa maaskofu wa Kikristo na wanazuoni wa Kiislamu Ufilipino

10:41 - November 19, 2008
Habari ID: 1710081
Mkutano wa maaskofu wa Kikatoloki na Kiprotestanti na wanazuoni wa Kiislamu ulianza kazi zake jana katika mji wa Jolo nchini Ufilipino.
Mwandishi wa IQNA ameripoti kuwa mkutano huo ni wa kihistoria kwa shabaha ya kueneza amani na mazungumzo kati ya dini nchini Ufilipino.
Gazeti la Gmanews la Ufilipino limeripoti kuwa moja ya ajenda za mkutano huo ni kutembelea maeneo ya kihistoria ya Ufilipino hususan sehemu ambako wahubiri wa kwanza wa Kiislamu walipofikia katika karne ya 13.
Ni vyema kukumbusha hapa kuwa asilimia tano ya jamii ya watu milioni 90 ya Ufilipino ni Waislamu 322267

captcha