Kikao hicho kimehudhuriwa na wanachama wa Taasisi ya Twawafu ya Mahujaji wa wa Ulaya, viongozi wa Wizara ya Hija ya Saudi Arabia, wakuu wa misafara ya Hija ya nchi mbalimbali na taasisi zinazosimamia ibada ya Hija.
Wail bin Saleh Halabi, afisa wa idara inayosimamia amali ya kupiga mawe nembo ya shetani amesema kuwa kikao hicho cha kila mwaka kimechunguza namna ya kuwaelimisha mahujaji jinsi ya kutekeleza ibada hiyo na taratibu zitakazotumiwa na makundi mbalimbali ya mahujaji wakati wa kutekeleza amali hiyo ya Hija.
Amesema, malengo mengine ya kikao hicho ni kuboresha huduma kwa mahujaji wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu, kujenga mawasiliano ya mara kwa mara kati ya ujumbe mbalimbali za Hija na viongozi wa serikali ya Saudi Arabia na kudhamini usalama na amani kwa mahujaji. 328870