IQNA

Qur'ani Tukufu kutotambuliwa kama chanzo kikuu cha sheria za katiba ya Libya

11:42 - December 18, 2008
Habari ID: 1720143
Viongozi wa Libya wameanza kuchunguza rasimu ya katiba mpya ya nchi hiyo kwa lengo la kuweka kando Qur’ani Tukufu na kutoitambua tena kama chanzo kikuu cha sheria za nchi na badala yake kutunga sheria zinazooana na demokrasia ya Kimagharibi.
Mtandao wa intaneti wa ‘mathaba.net’ umeandika kwamba, mtoto mkubwa wa kiume wa Kanali Muammar Gaddafi, Seiful Islam Gaddafi ameteuliwa kusimamia mchakato wa kutazama upya katiba ya nchi hiyo akishirikiana na wataalamu kutoka nchi za Ulaya na Marekani.
Qur’ani Tukufu imekuwa msingi wa katiba ya Libya tangu mwaka 1977 ambayo pia inategemea vipengee vya kitabu cha Green Book kilichoandikwa na Kiongozi wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi.
Uamuzi wa viongozi wa Libya wa kutoitambua Qur’ani kama chanzo kikuu cha sheria za katiba ya nchi hiyo umechukuliwa katika hali ambayo wananchi wote wa nchi hiyo ni Waislamu. 334359

captcha