Musib al Nuaimi ambaye pia ni mtaalamu wa masuala ya nchi za Kiarabu, amesema kuwa jumuiya za kimataifa kama Umoja wa Mataifa na mashirika yake, Benki ya Dunia na taasisi zenye mfungamano na jumuiya hizo za kimataifa ambazo zina makao Marekani, Geneva au katika nchi nyingine za Ulaya, zinadhibitiwa kikamilifu na madola makubwa kama Marekani.
Ameashiria mgogoro wa Palestina mbao ni changamoto kubwa ya jamii ya kimataifa na akasema: Mgogoro huo hauwezi kutatuliwa kwa kutegemea utendaji wa jumuiya za sasa za kimataifa na kwamba ni mapambano ya wananchi wa Palestina pekee ndiyo yatakayoleta ufumbuzi wa hali hiyo. al Nuaimi amesema kuwa taarifa zinazotolewa na nchi za Magharibi na jumuiya za kimataifa baadhi ya wakati kulaani jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel huko Palestina huwa na lengo la kuzihadaa fikra za waliowengi na kupotosha ukweli wa mambo.
Amelaani mzingiro wa Israel dhidi ya wakazi milioni moja na nusu wa Ukanda wa Gaza na akasema: Jinai hiyo inafanyika kwa uungaji mkono wa Marekani na nchi za Magharibi na haitakomeshwa isipokuwa kwa mapambano ya wananchi wa Palestina wenyewe na si kwa msaada wa jumuiya za kimataifa. 336761